airtel

airtel

.

.

Thursday, April 11, 2013

CONGRATULATION LOVELY BROTHER,MAY PEACE OF ALLAH UPON ON YOU AND YOUR BELOVED WIFE,HAVE A GOOD TIME

BE THE FIRST TO GET TO KNOW SHAA’S BIOGRAPHY

SHAA (real name Sarah Kaisi) is a 27 year old talented Bongo Flava and Afro Pop artist in every sense of the word. This daring vibrant Diva was born and raised in Dar es Salaam, Tanzania and grew up in a musical family which includes a brother and sister who are also musicians themselves.
Early 2004, under the group “WAKILISHA” of the East Africa Coca Cola Pop Stars, SHAA who was then known by her birth name Sarah made her debut into the Tanzania music scene. With their hit single “Hoi” SHAA and her fellow group members managed to win themselves a spot in the East Africa music industry.
However, in 2005 SHAA left the group and went to USA to further her studies in another passion of hers which is Art. It was during her studying period abroad, under the management of WAKILISHA’s previous manager, Daniel Kiondo of Kiondo Communications International , that SHAA started working on
her solo career.
In October 2008 SHAA's solo career finally kicked off when she landed herself a major record deal with a prominent record label in Tanzania, MJ Records. Under MJ Records, SHAA has managed to record and release many hits such as ZAMU YANGU (meaning MY TURN), PAMBAZUKA, a track that also featured AY, SHOGA (meaning MY FRIEND), CRAZY and many many more.
With such hits under her belt SHAA earned her first Tanzania Music Awards Nominations for best R&B artist in 2008, Best Female Vocalist and Best Female Artist in 2010 and Best Female Performer in 2011. She also earned herself her very first MAMA(MTV Base) Awards Nomination in the Best New Act
Category in 2009 and a Channel O Music Awards Nomination in the Best East African Act Category in 2010 and the Best Afro-Pop Act in 2011 where she went head to head with acts such as JMartins
and Mr.Flavour from Nigeria.
Although she didn’t manage to grab any of the awards her hard work finally paid off in late 2011 when her then hit SHOGA won the Best Afro-Pop song in the MUSEKE Awards beating out some of Africa’s best such as D’banj and 2Face Idibia.

Rick Ross’ Lyrics Spark Protest At A NYC Reebok Store

Rick Ross Re-Signs Promotional Deal With Diddy’s Ciroc Vodka

Rick Ross has recently been taking a lot of heat for the song “You Ain’t Even Know It” lyrics that many believe implies date rape. Now, though the rapper issued an apology via Twitter on Thursday, one activist organization feels the rapper’s words do not make full atonement, and is pushing that he endure more serious consequences.
Following the release of his tweet, the women’s rights group UltraViolet came together and rallied outside the Reebok flagship store in New York City demanding the sneaker company drop Ross as spokesperson.
“It’s time for Reebok to stop using their brand as a platform to dictate to women what counts as rape. Contrary to Ross’ claims, there was no misinterpretation here: Slipping a woman a drug and ‘enjoying that’ is rape, plain and simple,” says a statement on the company’s website by co-founder Nita Chaudhary. “It’s time for them to answer the 72,000 former customers who want them to stop promoting violence against women and fire Rick Ross.”
The organization has put together a petition and has collected more than 70,000 signatures from supporters who feel and agree Ross should be dropped from Reebok.
“It’s unacceptable that Reebok, one of the oldest brands in athletics, would stand behind someone who so openly condones rape. Companies like Reebok have a responsibility to the public,” says another statement issued on a press release by Sonia Ossorio, President of NOW NYC – an organization supportive of UltraViolet’s mission.
“Propping up someone who rants about rape and paying that person millions of dollars is about as irresponsible as it gets. The Reebok board of directors should take immediate action,” she added.

UHURU KENYATTA ALIHUTUBIA TAIFA LA KENYA AAHIDI USHIRIKIANO NA KUTOA AJIRA KWA VIJANA

HIVI NDIVYO MSANII KAJALA ALIVYOKARIBISHWA URAIANI PARTY LA NGUVU LASHUKIA



wema, kajala n friend wakishow love..

best friends forever inshaallah mwenyez mungu awaweke


hapa wakiingia ukumbini..

wema, dj fetty n kajala..

keki..

hayaweee mambo JD hayooo...



akizungumza machache kabla ajakata keki..

wema na yeye akiongea machache,,, kajala dont cry bhanaa...

keki hizooo..

yumm!!

wow.......



marafiki mbalimbali wakilishwa keki..

aunt na kajala..

bilali mashauzi, bilal wa A akila keki na yeye..

hapo chacha!! kajala akimlisha petit man keki..

yvone nae akila keki..

**WELCOME BACK KAJALA**

Tuesday, April 2, 2013

RAIS KIKWEETE AMTEMBELEA NAIBU RAIS WA KENYA WILLIAM RUTO

RAIS KIKWETE AKISALIMIANA NA RUTO
RAIS KIKWETE AKISALIMIANA NA RACHEL CHEBET MKE WA MAKAMU WA RAIS WA KENYA
WAKIBADILISHANA MAWAZO YA KUJENGA USHIRIKIANO
PICHA YA PAMOJA RAIS KIKWETE AKIWA NA FAMILIA YA RUTO

JENGO LA GOROFA 16 LILILOANGUKA DAR,WATAALAMU WAMELITOLEA MAELEZO NA WATOA SABABU ZAO ZA KITAALAMU ZISOME HAPA

Tathmini iliyoratibiwa kisayansi na timu ya waandishi wetu, ikihusisha baadhi ya wataalamu wa majengo, inaonesha kwamba aina ya ujenzi wa jengo hilo, ulikuwa haukidhi hata kwa ghorofa tano.
Jengo lililopo jirani na lile lililoporomoka.
Machi 29, mwaka huu (Ijumaa iliyopita), jengo hilo, lililopo kwenye makutano ya Barabara ya Morogoro na Mtaa wa Indira Ghandhi, lilianguka na kuibua wasiwasi mkubwa.
Kwa mujibu wa mhandisi wa majengo, Abel Kadali, anayemiliki kampuni yake, akiwa ni msomi mwenye shahada mbili, ujenzi wa jengo hilo, ulizungukwa na utani mwingi.
“Kwanza jengo refu kama lile linapokatika na kubomoka kisha eneo kugeuka kifusi kama hivi, maana yake ujenzi ulikuwa dhaifu kuanzia mwanzo hadi mwisho.
“Kama ujenzi ungekuwa mzuri, hili jengo hata kama lingeanguka, lisingesambaratika kama hivi. Hapa kuna kasoro za kiweledi. Ujenzi wa namna hii, huwa unatufanya tuonekane hatuwezi kazi,” alisema.

KASORO KATIKA SARUJI
Macho ya waandishi wetu yaliona lakini Kadali akafafanua kwamba ni kosa kubwa kujenga ghorofa, halafu ukabana saruji.
“Nikishika tofali, naona ni mchanga mtupu. Kwa kadirio la kitaalamu, inaonekana kila mfuko mmoja  wa saruji, ulitengeneza matofali 90. Maana ni mchanga mtupu.
“Kwa hiyo kosa la kwanza kabisa ninaloweza kuliona hapa ni matumizi ya saruji,” alisema Kadali.

NONDO DHAIFU
Kadali alifafanua kuwa nondo zilizotumika siyo za kujengea ghorofa lenye urefu huo.
“Nikiziangalia hizi nondo, naona kabisa hili jengo lilijengwa chini ya kiwango kuanzia kwenye msingi wake mpaka hapo lilipofikia na kuanguka. Sasa ni kwa nini lisianguke?
“Tunacheza na maisha ya watu. Nondo ni nyembamba sana, nikiziangalia, zinaonesha kuwa pamoja na wembamba wake, hazina ubora,” alisema Kadali.

TATIZO LA MALIGHAFI
Kuhusu ubora wa nondo, Kadali alisema kuwa inashangaza kuona zikikunjwa zinakatika.
“Hili ni tatizo la malighafi, lazima ukaguzi wa kina ufanyike kwenye viwanda vyetu, kuona ubora wa bidhaa zinazotengenezwa.
“Ni kweli nondo ni nyembamba lakini ukweli usipindishwe kuwa hata ubora wenyewe haupo. Ina maana zilitengenezwa kwa malighafi zisizokidhi viwango.
“Viwanda vyetu vinaunda nondo kwa kuyeyusha vyuma chakavu. Ni kosa kubwa. Wakati mwingine inakuwa siyo vyuma peke yake, bali ni mchanganyiko na ‘Alminiamu’,” alisema Kadali na kuongeza:
“Kama nondo inatengenezwa kwa kuchanganya chuma na Alminiamu, unatarajia kweli kupata nondo imara? Ifahamike kwamba kila madini na kazi yake.”

KOSA LA TBS
Kadali alisema kuwa kiwango dhaifu cha nondo na bidhaa mbalimbali nchini, ni matokeo ya Shirika la Viwango Tanzania  (TBS) kutofanya kazi zake ipasavyo.
“Kuruhusu nondo kama zile kuingia sokoni na kuuzwa kwa ajili ya ujenzi, ni tatizo. TBS lazima wasimame imara kuhakikisha wanafanya kazi yao kisheria, hivyo kuokoa maisha ya Watanzania,” alisema Kadali.

KOSA LA NHC
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), nalo limeingia lawamani kwa sababu kisheria, lenyewe lina haki katika umiliki wa jengo hilo lililoanguka.
NHC, linamiliki asilimia 25 ya hisa za jengo hilo, hivyo kitendo cha kuacha ujenzi holela, siyo tu kwamba limeshindwa kutimiza wajibu wake, bali pia linachezea rasilimali za Watanzania.

MAITI ZAFIKIA 34
Mpaka gazeti hili linaingia mtamboni, maiti zilizokuwa zimepatikana ni 30 na jitihada za kuendelea kusaka maiti zaidi zilikuwa zinaendelea.
Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema: “Uokoaji bado unaendelea, vyombo vyote vya dola vipo, pamoja na zana zote.”

WANANE WAKAMATWA
Kova alisema: “Mpaka sasa, polisi kanda maalum imeshawakamata watu wanane kuhusiana na kuanguka kwa ghorofa hilo.
“Waliokamatwa ndiyo waliohusika moja kwa moja, kuanzia michoro mpaka ujenzi. Kwa sasa nisingependa kuwataja majina kwa sababu uchunguzi unaendelea,” alisema Kova.
Kwa upande mwingine, Kova alisema: “Kipindi hiki tunaendelea na uokoaji, hatutarajii kupata majeruhi. Tunachofanya ni kuhakikisha tunapata maiti wote ili waweze kuzikwa kwa heshima zote kama binadamu.”

KUHUSU JENGO PACHA
Habari zinasema kuwa jengo hilo lililoanguka, lilikuwa na pacha wake, jirani kabisa na ilipo Hospitali ya Burhani. Kova amesema kuwa ujenzi wake umesimamishwa mara moja.
“Tuligundua kuwa mmiliki na mjenzi ni yuleyule, kwa hiyo tumechukua hatua za haraka sana kuzuia shughuli zote za ujenzi wa jengo hilo pacha,” alisema Kova.

USHAHIHI WA PICHA ZA MATUKIO YA WATU 20 WALIOFUKIWA NA KIFUSI,JIJINI ARUSHA HIZI HAPA,PAMOJA NA TAARIFA YAKE SOMA HAPA


Maelfu ya wakazi wa jiji la Arusha na viunga vyake wakishuhudia miili ya marehemu wakiopolewa kwenye kifusi baada ya kukatika ngema kubwa katika machimbo ya mgodi wa Moramu uliyopo Moshono jijini Arusha.

Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Kikosi cha Uokoaji cha Tanganyika Parkers, wakiopoa baadhi ya miili ya merehemu.
(Picha na Joseph Ngilisho,…
Maelfu ya wakazi wa jiji la Arusha na viunga vyake wakishuhudia miili ya marehemu wakiopolewa kwenye kifusi baada ya kukatika ngema kubwa katika machimbo ya mgodi wa Moramu uliyopo Moshono jijini Arusha.
Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Kikosi cha Uokoaji cha Tanganyika Parkers, wakiopoa baadhi ya miili ya merehemu.
WATU zaidi ya 20 wamefariki dunia kwa kufukiwa na kifusi wakati wakichimba  mchanga aina ya Moramu katika machimbo  yaliyopo Moshono nje kidogo ya jiji la Arusha.
Tukio hilo ambalo limegubikwa na simanzi na vilio kwa ndugu jamaa na wananchi, limetokea leo majira ya saa 5 asubuhi wakati marehemu hao wakichimba na kupakia Moramu hiyo kwenye magari .
Pamoja na vifo hivyo magari mawili aina ya Fuso na Scania yameharibiwa vibaya baada ya kufukiwa na kifusi kilichoporomoka umbali unaofikia mita 50 kutoka usawa wa bahari.
Tayari kikosi cha uokoaji ambao ni  Jeshi la Wananchi Kambi ya Tanganyika Parkers kimefanikiwa kuopoa miili ya marehemu 16 waliofukiwa.
Baadhi ya miili ya marehemu  imetambulika kwa majina kuwa ni  Alex Maliaki, Gerald Hamis, Sauli Rafael (Mbu), Barick Loselian, Kababuu Lowasale, Mwenda Kibobori, Japhet Mjivaine na Garald Masai.
Taarifa za mashuhuda zimebainisha kwamba chanzo cha kuporomoka kwa kufusi hicho ni mvua kubwa zinazoendelea kunyesha jijini Arusha zilizosababisha kukatika kwa Ngema baada ya kuzidiwa na maji ya mvua.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...