airtel

airtel

.

.

Wednesday, January 30, 2013

PICHA ZA MAJUMUISHO YA ZIARA YA DHARURA YA WAZIRI MKUU MKOANI MTWARA

DONDOO MUHIMU KATIKA MAJUMUISHO
  • Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Mstaafu Simbakalia kawaomba radhi wananchi wa Mtwara.
  • Waziri Nchimbi ameahidi suala la usalama ni la kila mmoja,amani na utulivu vinahitajika katika kujenga demokrasia ya kweli,pia jeshi lake litakuwa karibu na raia
  • Kawambwa kawahimiza wazazi kuwaruhusu watoto kwenda shule kupata elimu sanjari na chuo cha VETA kutoa masomo ya mitaala ya gesi sanjari na uchomeleaji baharini.
  • Tibaijuka amezungumzia kuhusu upanuzi wa mji wa Mtwara na kuleata kauli mbiu ya "Amani na maendeleo" kutoka kwao Kagera.
  • Mwakyembe amezungumzia  upanuzi wa bandari kavu na ujenzi wa reli Mtwara, Liganga, Mchuchuma hadi  Mbamba bay na kuahidi kuja Mtwara kila baada ya miezi 3 na kujadili na kutathmini changamoto.
  • Waziri Mkuu ametoa udhuru wa waziri wa ujenzi Dr Magufuli ambaye alitakiwa kuwepo lakini hataweza kuhudhuria.
  • Bi Mapunjo kaahidi mipango mikubwa ya ujenzi wa viwanda mkoani Mtwara.
  • Mbilinyi kaainisha idadi ya makampuni yaliyoonyesha nia ya kuja kuwekeza Mtwara
  • Waziri Mkuu katoa majumuisho ya ziara yake ambayo hayana tofauti na haya yaliyojadiliwa.
  • Nasta boy blogspot.com inaipongeza serikali kwa hatua hii ya kutafuta muafaka wa suala la gesi na ni matumaini kuwa wana mtwara watanufaika na rasimali hii muhimu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...