airtel

airtel

.

.

Friday, January 10, 2014

[Football] Yaya Toure Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Africa Mara 3 …



yaya
Mara baada ya masaa 24 kupita tokea timu yake ya klabu ya Manchester City kufanikiwa kuisambaratisha timu ya West Ham United kwa mabao 6 kwa 0 katika mashindano ya Capital One Cup huko Uingereza, mchezaji mpira mahiri wa Timu ya Taifa ya Ivory Coast na Manchester City ya Uingereza amefanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa Africa kwa maara ya tatu mfululizo, ambapo mahafali hayo yalifanyikia katika ukumbi wa Gala nchini Nigeria katika jiji kubwa la Lagos.
toure_2535905b
Kutokana na kiwango cha mchezaji huyo wa kati wa timu ya Man City na Ivory Coast, ambacho kimekuwa juu kwa muda mrefu ni sababu iliyomfanya mcezaji huyo kutwaa tuzo hiyo na pia mchango wake wakuweza kuifanikisha timu yake ya Taifa kufuzu kucheza mashindano ya World Cup yatakayofanyika South America Brazil. Wachezaji wengine waliofanikiwa kutwaa tuzo hiyo mara tatu mfululizo ni Abedi Pele wa Ghana na Samuel Etoo wa Cameroon ambapo Etoo alichukua 2003-05 na kuchukua kwa mara ya nne 2010.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...