airtel

airtel

.

.

Friday, October 2, 2015

HUAWEI Y360, KIKI INAYOPEWA INAFANANA NA UBORA WA SIMU HUSIKA.

Katika siku kadhaa zilizopita kumekuwa na matangazo kadhaa hasa kwenye mitandao ya kijamii juu ya simu mpya inayouzwa kwa ushirikiano wa makampuni mawili nguli ya mawasilino nchini. Huawei ambao ni watengenezaji wa simu kwa ushirikiano na Tigo.
Untitled
Baadhi ya watu maarufu wamekua wakiizungumzia kwenye kurasa zao binafsi. Kama unavyooa Dina Maris hapo juu. Kama mtandao wa masuala ya teknolojia, nikaona si mbaya kama tutaitazama simu husika, ili kujua kama YALIYOMO YAMO.
Simu hii inauzwa shilingi 160,000 kwenye maduka ya Tigo ambapo utarudishiwa pesa uliyonunulia kama vifurushi kwa miezi sita. Hii ni ofa nzuri kwa simu yenye sifa hizi.
Simu hii inatumia Android OS, v4.4.4 (KitKat), kioo cha inchi nne na CPU Quad-core 1.2 GHz Cortex-A7. Ina Camera mbili, ya mbele (maalumu kwa SELFIE) ina 2MP na ya nyuma ina 5 MP, 2592 х 1944 pixels, flash mbili.
2
Waswahili husema kizuri hakikosi kasoro, Je kuna kasoro gani nilizoona kwenye simu hii? Ukweli ni kwamba sikuona tatizo lolote. Bei yake ni ndogo sana ukifananisha na sifa za simu hii. Kama unahitaji simu bora kwa gharama nafuu basi hii ni simu kwa ajili yako.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...