airtel

airtel

.

.

Thursday, June 7, 2018

TAZAMA VIDEO HII ,Viongozi wa elimu Geita wakipatiwa mafunzo kukabiliana na Malaria

KIFO CHA SAM WA UKWELI,TAARIFA YOTE IPO HAPA KUPITIA MICHUZI TV

KIKOSI CHA JESHI LA ZIMAMOTO NCHINI CHAPATA TUZO YA UTENDAJI BORA

PIX%2B1
 Mkurugenzi wa Idara ya Jinsia, Wazee na Watoto wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA), Mohamed Shabani (wapili kulia) akimkabidhi Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye tuzo ya cheti cha heshima, kwa mchango wao katika kupambana na majanga ya moto na uokoaji. Hafla hiyo imefanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam. 
PIX%2B2
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye akionesha zawadi ya fulana ya mabalozi wa Taasisi ya Salama Salimini aliyokabidhiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Jinsia, Wazee na Watoto wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA), Mohamed Shabani (kushoto), kama alama ya kutambua mchango wao katika kupambana na majanga ya moto na uokoaji, (kulia) ni balozi wa Salama Salimini Mwinyi Mangara. Hafla hiyo imefanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
PIX%2B3
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye, akifafanua jambo kwa Waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kukabidhiwa tuzo ya cheti cha heshima kutoka kwa Idara ya Jinsia, Wazee na Watoto wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA), kwa mchango wao katika kupambana na majanga ya moto na uokoaji. Hafla hiyo imefanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
PIX%2B4
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (wa tatu kulia) akiwa na Viongozi Waandamizi wa Jeshi pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Jinsia, Wazee na Watoto wa Asasi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania (AWAMATA), Mohamed Shabani (wapili kushoto), (kulia) Kamishna wa Operesheni wa Jeshi hilo Billy Mwakatage, (kushoto) Kamishna wa Usalama Dhidi ya moto Jesuald Ikonko na (wapili kulia) ni balozi wa Salama Salimini Mwinyi Mangara. Hafla hiyo imefanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam. (Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji)
 
NA MWANDISHI WETU NURUDINI STAMBULI
 
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limepokea tuzo ya cheti cha heshima kwa kutambua mchango wao katika kupambana na majanga ya moto na uokoaji hapa nchini kutoka katika Taasisi ya Wazalendo na Maendeleo. Tuzo hiyo imepokelewa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye Makao Makuu ya Jeshi hilo yaliyopo Dar es salaam
Akizungumza Kamishna Jenerali baada ya kupokea tuzo ya cheti hicho. Alisema, anawashukuru Taasisi hiyo kwa kulipa Jeshi hilo tuzo hiyo kwa kazi nyingi ambazo taasisi hiyo imezifanya kwa kushirikia na Jeshi hilo ikiwepo kampeni ya kuitangaza namba ya simu ya dharura 114.
Kamishna Jenerali Andengenye, amezitaka Taasisi nyingine kushirikiana na Jeshi hilo katika kuzifufua Fire Hydrant zilizo haribika na zilizofukiwa ili kuongeza idadi ya vifaa hivyo ambayo ni msaada mkubwa wakati wa majanga ya moto. ‘‘Jamii ishirikiane na Jeshi letu katika kuvilinda visima hivyo (Fire Hydrant) vilivyopo mitaani kwani ni msaada mkubwa pale majanga ya moto yanapotokea’’.
Ni vema sasa mamlaka zinazoshughulikia miundombinu ya maji safi kwenye miji na majiji ikazingatia wanapotengeneza miundo mbinu hiyo, wakumbuke kuweka na mifumo ya maji ya zimamoto Fire Hydrant, pamoja na kuhakikisha wamiliki wanaojenga majengo makubwa na madogo wanaweka mifumo hiyo ya maji.
Tuna changamoto kubwa kwa upande wa visima hivyo, kwa hiyo kamapeni yetu ya kufufua na kuongeza visima hivyo vitasaidia kuleta tija katika utendaji kazi katika fani yetu. Tunashirikiana na Mamlaka za Maji kuhakikisha miundo mbinu hiyo inarudi na kutoa ushauri pale miradi mipya ya maji inapo jengwa.
Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Wazalendo na Maendeleo Tanzania Bw. Muhammad Shaban alisema wamechukua uamuzi huo wa kutoa Tuzo hiyo kutokana na kuona mchango mkubwa wa Jeshi hilo walioutoa katika jamii. Pia amesema wataendea kutoa ushirikiano na Jeshi hilo katika utoaji elimu kwa umma. “Tupo tayari kushirikiana na Jeshi hili kuwaonesha sehemu zote ambazo fire hydrant zilizopo Mkoa wa Dar es salaam.”
“Kampeni ya kufufua fire hydrant imetugusa sana na kuona hatua hiyo ni msaada mkubwa kwa jamii kwani zitasaidia magari ya zimamoto na uokoaji kupata maji eneo la karibu majanga ya moto yanapotokea.”

Tanzania Yang’ara Mifumo Ya TEHAMA Inayolenga Kuleta Ustawi

Tanzania imetajwa kuwa nchi iliyofanikiwa kuwa na mifumo bora ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) inayolenga kuchochea ustawi wa maisha ya wananchi hasa wanaoishi katika maeneo ya vijijini.
Akizungumza katika mahojiano maalum yaliyofanyika Jijini Mbeya leo, Mkuu wa Timu ya Mifumo ya Mawasiliano wa Mradi wa Kuimarisha Mifumo ya Sekta za Umma  (PS3) Bw. Desderi Wengaa, amesema kuwa hivi sasa Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano kwa kuwa na mifumo bora na inayoongea, hali inayosaidia kuimarisha huduma kwa wananchi hasa wanyonge. 
PS3 ni mradi unaofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).  Mradi huu wa miaka mitano unatekelezwa katika mikoa 13 ya Tanzania bara.
“Mifumo hii inalenga kuwawezesha watoa huduma katika ngazi ya vituo vyao kama Zahanati, Shule na Vituo vya Afya kutoa huduma kulingana na mahitaji ya wananchi na vipaumbele vya Serikali ambavyo kimsingi vinalenga kuwaletea wananchi maendeleo endelevu,” alisisitiza Wengaa.
Akifanua, Bw.Wengaa amesema kuwa mfumo kama wa Epicor 10.2 utasaidia Serikali kujua mapato na matumizi ya fedha za umma katika sekta za kipaumbele kama Afya na Elimu, ikiwa ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kuwa rasilimali zote, ikiwemo fedha zinatumika kuboresha maisha ya wananchi.
Ameongeza kuwa kwa kutumia mifumo hiyo, thamani halisi ya fedha zitakazotumika katika miradi ya maendeleo itaonekana na pia itaongeza muda wa kuwahudumia wananchi katika vituo vya kutolea huduma, kwakuwa muda utakaotumika kwa kila anayehitaji huduma kuwa mchache.
Akieleza mikakati ya kufanya mifumo hiyo ilete matokeo tarajiwa, Bw. Wengaa amesema kuwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kushirikiana na PS3 watakuwa na dawati la kufuatilia na kuhakikisha kuwa mifumo yoye inafanya kazi na kuleta matokeo tarajiwa.
Akizungumzia moja ya mfumo unaotumika katika sekta ya afya (Government of Tanzania Hosipital Management System – GoT-HoMIS) amebainisha kuwa unasaidia kutunza kumbukumbu za mgonjwa kuanzia siku ya kwanza anapofika kupata huduma, hivyo kuisaidia Serikali katika kutambua mahitaji halisi katika maeneo husika na hivyo kuboreshwa kwa huduma zinazotolewa.
Wakati Mfumo mwingine ni ule unaotumika katika kupanga mipango, bajeti na kutoa taarifa (PlanRep) ambao unasaidia watendaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kuandaa mipango na bajeti katika vituo vyao na kuiwasilisha Ofisi ya Rais – TAMISEMI, kupitia mfumo huo, hivyo kuokoa rasilimali fedha na muda uliokuwa unatumika awali kuandaa mipango na bajeti hizo.
Tanzania kutajwa kuwa nchi ya kupigiwa mfano ni kutokana na pia kuwepo kwa mifumo kama ile ya kubaini mahitaji ya watumishi katika sekta ya afya, hasa katika vituo vya kutolea huduma na vipaumbele vya eneo husika.
Kuhusu mifumo hiyo kuongea, Wengaa amebainisha kuwa, hali hiyo itasaidia kubainisha uwiano wa majukumu kati ya mtumishi mmoja na mwingine katika vituo vya kutolea huduma za afya, hivyo kubaini watumishi wanatekeleza majukumu mengi zaidi kuliko inavyotakiwa ili kuweza kuongeza watumishi wengine katika eneo hilo. 
Baadhi ya mifumo hiyo ni PlanRep, WISN na POA, GoT-HoMIS na mfumo wa kuandaa taarifa za uhasibu katika ngazi ya kutolea huduma (FFARS), ambayo iko chini ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.  WISN na POA inasimamiwa kwa pamoja na Ofisi ya Rais Utumishi, ikiwa ni moja ya hatua zinazochukuliwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kuboresha huduma za afya hapa nchini.
IMG_4183
Mkuu wa Timu ya Mifumo ya Mawasiliano wa Mradi wa Kuimarisha Mifumo ya Sekta za Umma  (PS3) Bw. Desderi Wengaa akisisitiza kuhusu umuhimu wa mifumo hiyo katika kuwaletea wananchi maendeleo, wakati wa mahojiano maalum leo Jijini Mbeya

WAZIRI WA ELIMU AWATAKA WATANZANIA KUISHI KWA KUPENDANA



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia amewataka watanzania kujenga tabia ya kupendana, kuvumilia na kuhurumiana katika maisha ya kila siku.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo leo mkoani Iringa mara baada ya kuongoza mamia ya wananchi wakati wa ibada ya kuaga miili ya mapacha walioungana Maria na Cosolata katika viwanja vya Chuo Kikuu Cha RUAHA mkoani Iringa.   

Amesema Maria na Consolata katika uhai wao waliishi wakiwa wameungana kwa hiyo waliishi kwa kuvumiliana na kupendana pia.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiaga miili ya mapacha walioungana Maria na Consolata katika viwanja vya Chuo Kikuu cha RUAHA Mkoani Iringa.

Amesema, Watanzania wanatakiwa kujiuliza kwa nini Maria na Consolata wamezaliwa Tanzania na Siyo nchi nyingine? amesisitiza kuwa watoto hao wamezaliwa nchini hapa ili iwe funzo kwa watanzania.

Maria na Consolata watazikwa kwenye jeneza moja litakalokuwa na misalaba miwili.
Maria na Consolata Mwakikuti walifariki jumamosi saa mbili usiku Juni 2 mwaka huu na miili yao itapumzishwa kwenye nyumba yao ya milele kwenye makaburi ya viongozi wa Kanisa Katoliki Tosamaganga mkoani Iringa.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akilia kwa huzuni mara baada ya kuaga miili ya mapacha walioungana Maria na Consolata katika Viwanja vya Chuo Kikuu cha RUAHA Nkoani Iringa.

Kwa upande wake sista Calista Ludega ambaye ni Mkuu wa Shirika la Mtakatifu Theresa wa Mtoto wa Yesu Jimbo Katoliki la Iringa amesema kuwa wamewazika Maria na Consolata mahala wanapolala Masista wa Maria Consolata kwa ajili ya kuwaenzi masista wa Wamishionari wa Consolata kwa kuwa wao wamekuwa sehemu kubwa ya malezi tangu waliopozaliwa watoto hao hadi wanapomaliza maisha yao duniani.

Familia ya Baba na mama wa mapacha hao kutoka Mkoani Mbeya na Kagera, masista wa Consolata wa Iringa na waombolezaji wengine wameungana katika kuwasindikiza katika safari yao ya mwisho duniani.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiweka saini kitabu cha maombolezo ya Msiba wa mapacha walioungana Maria na Consolata.

Thursday, December 21, 2017

WANAFUNZI 1,300 WA S/M NA SEKONDARI MKOA WA PWANI WAMEACHA SHULE KWA MWAKA 2014/2017-RC NDIKILO


IMG_20171208_111849
Baadhi ya viongozi na wadau wa elimu mkoani Pwani wakimsikiliza mkuu wa mkoa huo mhandisi Evarist Ndikilo ,wakati alipokuwa akizungumza masuala ya elimu na changamoto zinaxokabili sekta hiyo ,kwenye ukumbi wa mikutano uliopo katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani
IMG_20171208_111648
Mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo, akizungumza jambo kuhusu masuala ya sekta ya elimu na changamoto inazozikabili kwa viongozi na wadau mbalimbali wa elimu mkoani hapo kwenye ukumbi wa mikutano katika ofisi za jengo la mkuu wa mkoa . 
Picha na Mwamvua Mwinyi
…………..
Na Nurudini stambuli,Pwani
SERIKALI mkoani Pwani ,imeweka bayana kuwa,jumla ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari 1,300 wameacha shule (mdondoko),kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2014-2017,hali inayosababisha kukosa haki yao ya elimu.
Aidha kumekuwa na tetesi kwamba baadhi ya watoto hao wanaoacha shule hujihusisha na vikundi vya uhalifu ndani na nje ya mkoa huo ,jambo ambalo linahitaji nguvu za pamoja kulikomesha tatizo hilo.
Pamoja na hilo ,imeeleza kumekuwepo na tatizo la uzembe kwa baadhi ya wasimamizi wa elimu kutotekeleza ipasavyo majukumu yao,;:na pia kutofikiwa kwa malengo ya uandikishaji wa elimu ya awali na darasa la kwanza na udahili wa kidato cha kwanza hivyo kusababisha watoto wenye umri wa kwenda shule kutokwenda shule.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani,mhandisi Evarist Ndikilo,aliyasema hayo wakati akizungumzia changamoto na masuala ya sekta ya elimu mkoa,kwa viongozi wa Idara ya elimu mkoani hapo, wakurugenzi,wakuu wa wilaya na wadau wa elimu.
Alielezea ,kati ya watoto hao 1,300 wanaodaiwa kuacha shule kwenye mkoa mzima ,kwa upande wa wilaya ya Rufiji ni wanafunzi 381 na Kibiti ni 110 .
“Niliwahi kuomba taarifa ya mdondoko kwa kipindi cha mwaka 2014-2017 kutoka kwa wakuu wa wilaya zote “
“Ambapo mkoa wa Pwani una jumla ya shule za msingi 613 na sekondari 174 ,ndipo nilipoletewa idadi hiyo ambayo kiukweli ni chanzo cha kuporomoko  kwa taaluma mkoani hapo” alisema mhandisi Ndikilo.
Mhandisi Ndikilo aliagiza wanafunzi wote walioacha shule na watoro watafutwe ,warudishwe shule kisha wazazi na walezi wachukuliwe hatua za kisheria ikiwepo kufikishwa mahakamani kwa kushindwa kufuatilia mahudhurio ya watoto hao.
Alibainisha lipo tatizo jingine la mimba kwa watoto wa kike ,upungufu na uchakavu wa miundombinu ya shule ikiwemo madarasa ,nyumba za walimu ,matundu ya vyoo,ofisi za walimu, maabara na hostel.
Mkuu huyo wa mkoa, alisema kwasasa shule za msingi kuna mahitaji ya vyumba vya madarasa 7,609 ,vilivyopo ni 4,010 hivyo upungufu ni madarasa 3,599.
Mahitaji ya nyumba za walimu ni 6,328 ,zilizopo ni 1,592 ,upungufu ni nyumba 4,736 ,matundu ya vyoo yanayohitajika ni 13,750 ,yaliyopo ni 5,375 upungufu ni matundu 8,375 .
Mhandisi Ndikilo alitaja mahitaji ya vyumba vya madarasa katika shule za sekondari mkoani Pwani kuwa ni 1,479 ,vilivyopo ni 1,366 ,upungufu ni 113 ,mahitaji ya nyumba za walimu 3,684 zilizopo 671 hivyo upungufu 3,013.
Matundu ya vyoo yanayohitajika ni 2,405 yaliyopo ni matundu 1,961,upungufu ni matundu 444 ,na mahitaji ya maabara ni 333 yaliyopo ni 195 na upungufu ni 138.
Hata hivyo ,Mhandisi Ndikilo alizitaka halmashauri mkoani humo ,ziande mkakati wa kujenga hostel katika kila shule ya sekondari ili kuwalinda watoto hasa wa kike wanaotembea umbali mrefu kwenda na kurudi shule.
Sanjali na hilo ,ziwe na mpango mkakati wa kujenga na kukarabati miundombinu ya shule ikiwemo vyumba vya madarasa ,matundu ya vyoo na nyumba za walimu na kukamilisha ujenzi ifikapo 2020 .
Alitoa wito kwa wadau wa elimu kuunga mkono juhudi za serikali ya mkoa katika ujenzi wa miundombinu katika shule za msingi na sekondari.
Katika hatua nyingine ,mhandisi Ndikilo alisema lengo la serikali ni kuimarisha sera ya viwanda ili kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025 ,na msingi mkubwa wa sera hiyo ni elimu.
Aliwataka wakuu wa wilaya, wakurugenzi, watendaji wa halmashauri pamoja na watendaji wengine kuhakikisha wanafunzi wanaodahiliwa kidato cha kwanza wanasimamiwa hadi wanamaliza kidato cha nne ili waweze kushiriki katika kuimarisha uchumi wa viwanda.
Alisema kwamba,watoto wasipopewa elimu ,maarifa na ujuzi mahsusi watakuwa watazamaji badala ya watendaji licha ya mkoa huo kusheheni viwanda.

Wednesday, December 20, 2017

RAIS MAGUFULI ABAINI MADUDU KATIKA MKATABA WA AIRTEL NA TTCL

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjDr32KGzKHoPwhkwmZEfS6OESJs03puPp3GR2DZTrbK7BNwgqtQZ43V4deZ90-xtnFB4l8mtTedoC-mGso8_S9cJlE_NDSXCcPwfTQODNtc_yrx_PGP4-LshQeubQDEn3428gzkA5RfaIa/s1600/1.jpg 
 RAIS John Magufuli amesema Serikali imebaini kuwa kampuni ya Mawasiliano ya Bharti Airtel ni mali ya Shirika la Mawasiliani Tanzania (TTCL) na amemwagiza Waziri wa fedha na mipango kufuatilia suala hilo haraka ili Airtel irudishwe kumilikiwa na serikali.Rais ameyasema hayo leo Desemba 20 wakati akizungumza kwenye Ofisi za Taifa za Takwimu mjini Dodoma.“Kampuni ya AIRTEL imethibitika kuwa ni mali ya Shirika la TTCL, lakini kuna mchezo ulifanyika, sasa sitaki kuongea sana. Nataka Waziri wa Fedha ufuatilie suala hili kabla ya mwaka huu kuisha,” amesema Magufuli.Taarifa na ndani zinabainisha kwamba hisa za Airtel zinatarajiwa kukabidhiwa kwa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na kuendesha biashara za kampuni hiyo yenye wateja wengi zaidi nchini ikiwa nyuma ya Vodacom na Tigo.Chanzo cha mpango huo kinatajwa kuwa ni uongozi wa juu wa TTCL uliotaka Serikali kudai haki zake za uwekezaji ndani ya Airtel ambako inaimiliki kwa ubia wa asilimia 40 kwa 60 na mwekezaji.Taarifa zinaarifu kuwa TTCL itamiliki hisa zote za Airtel Tanzania Limited ambapo tayari TTCL imewasilisha hoja ya kutaka kufanya hivyo baada ya kubaini kwamba Serikali ilipunjwa kwenye hesabu za uwekezaji. Hoja ya TTCL inaanzia Novemba 3, 1998 ilipoanzisha kampuni tanzu ya Cellnet ambayo ilifanya kazi mpaka Mei 7, 2001 ilipobadilishwa jina na kuitwa Celtel Tanzania huku umiliki wake ukiendelea kuwa chini ya shirika hilo kwa asilimia zote baada ya kuwekeza Dola milioni tano za Marekani (zaidi ya Sh11 bilioni sasa).Lakini, Januari 31, 2002, Celtel ikiwa chini ya umiliki wa TTCL ilikopa kiasi cha Dola 82 milioni (zaidi ya Sh180.4 bilioni) ili kukuza mtaji wake.Kwa kipindi hicho, TTCL iliyokuwa na thamani ya Dola 600 milioni (zaidi ya Sh1.32 trilioni) ilikuwa inamilikiwa kwa ubia kati ya Serikali na Kampuni ya Mobile System International (MSI) ya Uholanzi. Serikali ilikuwa inamiliki asilimia 65 ya hisa zote na mbia huyo asilimia 35 zilizosalia.Agosti 5, 2005, mabadiliko yalifanywa kwenye bodi ya wakurugenzi wa Celtel kwa lengo la kuunda kampuni mbili tofauti; Celtel ikitenganishwa na TTCL. Kutokana na mabadiliko hayo, Celtel iliwekwa chini ya umiliki wa MSI ambayo Septemba 2007 iliuza hisa zake kwa Zain ambayo nayo ilikuja kuziuza kwa Bharti Airtel, Juni 8, 2010.Imeelezwa kuwa TTCL inadai uwekezaji wake ilioufanya Celtel baadaye Airtel ambayo thamani yake imeongezeka maradufu sasa haulingani na inachokipata hivyo kutaka kusimamia biashara za kampuni hiyo ya mawasiliano.Hoja ya madai hayo ni namna umiliki wa hisa ulivyobadilishwa baada ya Celtel kutenganishwa na TTCL ambayo ilipewa hisa chache tofauti na ilivyostahili.Kwa sasa, Airtel Tanzania inamilikiwa na Serikali yenye asilimia 40 na Celtel Tanzania BV, kampuni tanzu ya Zain Africa BV ambayo ilinunuliwa na Bharti Airtel International, Novemba, 2010 ikiwa na asilimia 60.Katika mabadiliko yaliyofanywa hivi karibuni, Serikali iliilipa Bharti Airtel Sh14.7 bilioni hivyo kuchukua asilimia 35 ya hisa ilizokuwa inamiliki na kuifanya imiliki asilimia zote za TTCL.Sheria mpya iliyopitishwa hivi karibuni na Bunge imeibadili TTCL inayohudumia asilimia 0.82 ya soko kuwa shirika la umma la mawasiliano na kulipa jukumu kubwa katika sekta ya mawasiliano nchini.Bharti Airtel inatakiwa kuorodhesha asilimia 25 ya hisa zake katika Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE) ili kukidhi vigezo vya sheria ya posta na mawasiliano ya mwaka 2010, lakini bado haijafanya hivyo.



TUME MPYA YAUNDWA KUCHUNGUZA MALI ZA CCM NCHI NZIMA

Taarifa iliyotolewa December 20 2017 kuhusu yaliyojiri katika Kikao Cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kikao cha kwanza baada ya Mkutano Mkuu wa Taifa wa Tisa wa Mwaka 2017 imeeleza kuwa Rais Magufuli ameunda Tume ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) itakayokuwa na jukumu la kwenda kufuatilia Mali za Chama kote nchini Tanzania.
Wafuatao wameteuliwa kuwa katika Tume ya CCM ya kufuatilia na kuhakiki Mali za Chama; -
1. Dkt. Bashiru Ali Kakurwa – Mwenyekiti wa Tume
2. Walter Msigwa – Mjumbe
3. Albert Msando – Mjumbe
4. Galala Wabanhu (Hananasif) – Mjumbe
5. Albert Chalamila – Mjumbe
6. William Sarakikya – Mjumbe
7. Komanya Kitwara – Mjumbe
8. Dkt. Fenela Mkangara – Mjumbe
9. Mariam Mungula – Mjumbe
Tume hii itafuatilia mali za Chama kokote ziliko na itamhoji kila mtu anayehusika katika Chama na katika Serikali.

Sunday, July 2, 2017

GEITA KINARA WA MICHEZO

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akimkabidhi kombe mwanafunzi ambaye amewakilisha mkoa wa Geita katika michezo hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Butimba, mkoani Mwanza.

Saturday, July 1, 2017

FATNA RAMOLE MTANGAZAJI WA AZAMN TV HAJULIKANI ALIPO KAMA UMEMUONA POPOTE,SOMA HAPA

 Image may contain: 1 person


Una taarifa zozote kuhusu Fatna Ramole? @fatnaramole
Mfanyakazi mwenzetu @azamtvtz hajulikani alipo.
Unaweza kutoa taarifa zake kwa namba hii
0719669749
Asante. @ Dar es Salaam, Tanzania

MASTAA MBALIMBALI WA SOKA WAHUDHURIA NDOA YA LIONEL MESSI JUNE 30,2017

MESSI AVUNJA UKIMYA ACHUKUA JIKO RASMI








Usiku wa Ijumaa ya June 30 staa wa soka wa kimataifa wa Argentina anayeichezea FC Barcelona ya Hispania Lionel Messi alifunga ndoa na mpenzi wake wa toka utotoni Antonella Roccuzzo ambaye pia wamezaa nae watoto wawili wa kiume.













Messi na Antonella Roccuzzo walifahamiana toka Lionel Messi akiwa na umri wa miaka mitano na Antonella Roccuzzo ambaye ni mke wake kwa sasa akiwa na umri wa miaka 4, wameamua kufunga ndoa kwao Argentina ndoa ambayo ilihudhuriwa na wachezaji wenzake na marafiki zake mbalimbali.
Zaidi ya marafiki wa Lionel Messi wanaofikia 250 walisafiri kwa ndege binafsi kuelekea Argentina kuhudhuria harusi ya staa huyo ambayo simu za mkononi zilikuwa zimefungiwa kufanya kazi ndani ya ukumbi sherehe ilipo kwa lengo la kuweka privacy pamoja na ulinzi wa askari zaidi ya 450.


Rapper wa Marekani, Future amethibitisha show yake ya Tanzania, Julai 22.

TANZANIA YATAJWA KATIKA ZIARA YA MSANII WA MAREKANI FUTURE



future

Future ametoa orodha ya ziara yake ya muziki ya ‘The Future Hendrxx Tour’ na Tanzania ni moja ya nchi ambayo Tour hiyo itatembelea.
Future atatumbuiza Tanzania pamoja na Diamond Platnumz, Vanessa Mdee, Navy Kenzo na Weusi.

BEI MPYA ZA MAFUTA KUANZA LEO JULAI 1,2017






Ikiwa tunaanza mwezi julai leo, kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji EWURA ambao wametangaza kushuka kwa bei mpya za mafuta ya vyombo vya moyo ikiwemo magari na mashine. Bei hizi elekezi zimeanza kutumika rasmi leo July 1, 2017.
Nimekuwekea hapa chini bei za mafuta kwa nchi nzima kuanzia kesho Jumamosi July 1, 2017.

Thursday, June 29, 2017

HARAKATI ZA UKOMBOZI NA UTENDAJI WA KUSIMAMIA MISINGI YA UTAIFA

NUKUU YA LEO

KUNANI KENYA KUTOIKUBALI GESI YA TANZANIA

Picha inayohusiana                                                                                 Serikali ya Tanzania imelalamika kuhusu hatua ya Kenya kukataa kuruhusu wafanyibiashara wa Tanzania kuuza gesi ya kupikia nchini Kenya.

Kulingana na taarifa iliotolewa na katibu wa kudumu katika wizara ya biashara na uwekezaji Profesa Adolf Mkenda, serikali imegundua kupitia vyombo vya habari mjini Nairobi kwamba Kenya imepiga marufuku uingizaji wa gesi ya kupika kutoka Tanzania kupitia mpaka wa Kenya na Tanzania.
Profesa Mkenda alisema hatua hiyo ya Kenya ni kinyume na makubaliano ya jamii ya Afrika mashariki na makubaliano yalioafikiwa na mataifa hayo mawili baada ya taifa hilo kuiwekea marufuku Tanzania mnamo mwezi Mei 18, 2017.
Kulingana na Profesa Mkenda, hatua hiyo ya Kenya itaathiri wafanyibiashara wakubwa wa kibinafsi na raia wa kawaida ambao hujipatia kipato kupitia biashara ya kuuza gesi .
Alisema kwamba wakati wa mkutano wa Jamii ya Afrika mashariki ambao uliwaleta pamoja mawaziri wa biashara na viwanda swala hilo lilijitokeza.
Amesema kuwa iliamuliwa wakati wa mkutano huo ambao ulifanyika mwezi Juni tareh2 2017 kwamba Kenya ilifaa kuondoa marufuku ili kuafikia makubaliano hayo ya Afrika mashariki.
Wakati wa mkutano huo Kenya ilikubali kuondoa marufuku ya ununuzi wa gesi kutoka Tanzania kupitia mpaka wa mataifa hayo mawili.
Mbali na marufuku hiyo Kenya pia imeiwekea Tanzania marufuku ya ununuzi wa ngano swala ambalo kulingana na Mkenda ni kinyume na makubaliano ya biashara ya Afrika Mashariki.
Hatahivyo amesema kuwa serikali itaendelea na mpango wa kutatua tatizo hilo.
Hatahivyo katibu huyo hakusema ni hatua gani zilizochukuliwa na serikali ya Tanzania kufikia sasa.
Kulingana na gazeti la The Citizen nchini Tanzania, Siku ya Jumatatu katibu maalum nchini Kenya Andrew Kamau alisema kuwa wafanyibiashara hawataruhusiwa kununua gesi kupitia mipakani katika kipindi cha juma moja.
Hatua hiyo kulingana na Kamau ililenga kuzuia kampuni haramu zinazouza gesi ambazo zimeathiri usalama wa taifa hilo.
Katibu huyo aliandikia barua shirika linalodhibiti kawi na shirika la ukadiriaji ubora wa bidhaa KBS na kusema kuwa gesi yoyote ya kupikia inayoingia nchini ni sharti ipitie Mombasa ili kubaini ni wafanyibiashara gani ambao hawana kibali cha kuendesha biashara hiyo.

JE UMESAHAU PATTERN KATIKA SIMU YAKO,ELIMIKA HAPA

Njia hii ni mahususi kwa simu za android pekee, kwani ukifanya hivi katika simu nyingine haitafaa.

1.Zima simu yako

2.Bonyeza kwa pamoja kitufe cha kuwashia simu (Power Button) na kitufe cha juu cha kuongezea sauti (Volume Up Button) kwa sekunde 5 hadi uone simu inawaka.

3.Kwa watumiaji wa simu za Samsung Galaxy bonyeza kwa pamoja kitufe cha kuwashia simu (Power Button) na kitufe cha juu cha kuongezea sauti na Home button.

4.Utaona maandishi madogo upande wa kushoto  yaliyopangwa kushuka chini.

5.Bonyeza kitufe cha chini cha sauti ili kuchagua maneno yaliyoandikwa (Wipe data/Factory reset)

6.Kisha bonyeza kitufe cha kuwashia simu (Power Button).

7.Acha simu yako ifanye reboot.

8.Tayari umefanikiwa kuondoa password au pattern uliyoisahau.


UNASUMBULIWA NA MAUMIVU YA TUMBO,HII HAPA ELIMU YA KUKABILIANA NA TATIZO

Maumivu ya tumbo ni dalili inayosumbua watu wengi kwa wakati na umri tofauti. Karibu kila mtu katika maisha yake atapata namna fulani ya maumivu ya tumbo. Kuna sababu mbalimbali zinazosababisha maumivu ya tumbo na mara nyingi huwa sio za kutisha, hutubiwa na kupona. Mara chache husababishwa na hali ambazo zinaweza kuhatarisha maisha yako. Maumivu yanaweza kuwa katika sehemu maalum ya tumbo au tumbo zima.

Maumivu Ya Tumbo
Ni vizuri ukijua aina ya maumivu ya tumbo unayopata pamoja na dalili zinazoambatana nayo. Hii itasaidia kujua sababu ya maumivu na katika matibabu. Maumivu ya tumbo yanaweza kuwa maumivu ya kuchoma, kuungua, kukandamiza, kukata au. Yanaweza kuwa yanakuja na kuacha baada ya muda fulani. Pia yanaweza kuambata na dalili nyingine kama kutapika, kuharisha, kukosa choo, kupata choo chenye damu, tumbo kuvimba na homa.

Sababu za Maumivu ya Tumbo
Kuna hali nyingi zinazoweza kusababisha maumivu ya tumbo. Chanzo cha maumivu hutegemea na sehemu maumivu yalipo.

Maumivu chini ya mbavu kulia yanaweza kusababishwa na
• Mawe kwenye mfuko wa nyongo
• Maambukizi kwenye mfuko wa nyongo (cholecystitis)
• Uvimbe wa ini
• Jipu kwenye ini
• Homa ya ini
• Saratani ya kongosho na kifuko cha nyongo.

Maumivu chini ya chembe ya moyo
• Vidonda vya tumbo
• Kiungulia
• Saratani ya tumbo
• Saratani ya kongosho

Maumivu Pembeni mwa kitovu
• Mawe ya figo (kidney stones)
• Maambukizi ya figo (pyelonephritis)
• Maambukizi kidoletumbo (Acute appendicitis)

Maumivu chini ya kitovu
• Maambukizi ya mfumo wa mkojo
• Magonjwa ya zinaa kama klamidia, PID
• Vivimbe vya mji wa uzazi
• Mimba kuharibika
• Saratani ya kibofu cha mkojo
• Premenstrual Syndrome – PMS

Sababu nyingine za maumivu ya tumbo ni;
• Irritable bowel syndrome
• Utumbo kujiziba (intestinal obstruction)
• Utumbo kujisokota (volvulus)
• Food poisoning
• Allergy ya chakula
• Ugonjwa wa Crohn (Crohn’s disease)
• Ngiri (hernia)
• Homa ya tumbo (typhoid fever)

Kama unapta maumivu makali sana ya tumbo, yanajirudia au yanambatana na dalili zozote kati ya zifuatazo basi onana na daktari mapema iwezekanavyo.
• Homa
• Kutapika matapishi yenye damu
• Kutapika sana
• Kukosa choo hasa ikiambatana na kutapika
• Tumbo kuvimba
• Kama umeumia

Matibabu
Maumivu ya tumbo hutibiwa kutokana na sababu ya maumivu. Wakati ukielekea hospitali kwa ajili ya matibabu unaweza kutumia dawa za kutuliza maumivu kama paracetamol au diclofenac.

Ukifika hospitali mtaalamu wa afya atachukua historia ya ugonjwa wako na kisha kufanya uchunguzi pamoja na vipimo vitakavyokuwa muhimu kutokana na aina ya maumivu unayopata.

Kuna njia mbalimbali za matibabu za matatizo yanayosababisha maumivu ya tumbo, ikijumuisha dawa za kunywa au kuchoma na upasuaji.

MABALOZI WA USALAMA BARABARANI R.S.A TANGA WATOA ELIMU MUHEZA

Ndugu edom mwakimwagile akitoa elimu ya usalama barabarani
HATUTAKI AJALI TUNATAKA KUISHI 

Friday, April 1, 2016

MAKALA YA WIKI HII NA MWALIMU STAMBULI

MKINGA
WALIMU WA WILAYA YA MKINGA NA CHANGAMOTO ZA KUIBUA MBINU MPYA ZA MATUMIZI YA TEHAMA KATIKA UFUNDISHAJI,
NA: MWALIMU STAMBULI
Serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania,imekuwa na dhamira ya dhati ya kuhakikisha Elimu inakuwa kwa kiwango kikubwa na hasa katika uwekezaji mkubwa katika Sekta ya TEHAMA,kwa kuhakikisha mazingira bora na fursa za kitehama zinazokjitokeza zinatumiwa vyema na watumishi wa kila idara ikiwemo idara ya ELIMU,ambayo kutokana na umuhimu wake hakuna budi ya wadau na wanaosimamia Elimu katika wi;laya ya mkinga kuhakikisha wanahimiza matumizi ya istilahi na kutumia programu kadhaa za kompyuta  ambazo zitajanibishwa kwa kiswahili mfano window 7 ya kiswahili ambayo imekuwa mhimili mkubwa katika kurahisisha ufundishaji katika shule za msingi Tanzania imekuwa na watumiaji wachache au walimu wachache wanaotambua jinsi ya kuitumia vyema katika kufundisha.
Blog hii inatoa Rai kwa wilaya ya mkinga kuweka uwekezaji mkubwa katika kukuza TEHAMA ambayo inaweza kusaidia kwa kiwango kikubwa kuwajengea stadi wanafunzi  wetu ambao wameonekana kuwa na ari kubwa katika somo hili.

Wednesday, January 6, 2016

HAPPY BIRTHDAY MR.BEAN


Jina lake kamili ni Rowan Atkinson, raia wa Uingereza ambaye ni staa wa movie na comedy pia duniani !!
Unajua kitu kizuri kwa Mr. Bean anafanya comedy ambayo hata kama huelewi lugha yake, vitendo vyake tuu lazima akuache hoi kwa kicheko.
Leo Rowan Atkinson a.k.a Mr. Bean anasherehekea siku yake ya kuzaliwa akiwa anatimiza miaka 60… jamaa ni msomi pia mwenye Master’s Degree ya Electric Engireering.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...